Lucy ni nani?
|
Nilikuja hapa Uswisi miaka 24 iliyopita. Nimekuwa hapa katika mji uliojawa na kitamaduni wa Basel tangu 2009.
Jina langu ni Lucy Oyubo Osterwalder. Ninatoka Busia, Kenya. Busia iko karibu sana na Ziwa Victoria iliyo na ukubwa kama mara kumi hivi ya nchi hii ya Uswisi. Kwa kuwa siku zote nimekuwa na uhusiano mkubwa na utamaduni na lugha yangu, ninajivunia sana kufundisha lugha ninayojivunia sana ya Kiswahili hapa Basel na pia kwa kupitia njia ya mtandao dunia nzima. Kwa kuwa hakuna shule nyingine inayofungamanisha Utamaduni isipokuwa Hakuna Matata Crew, nimeifanya kuwa dhamira yangu kukufahamisha kikweli kuhusu utamaduni na lugha ya Afrika Mashariki. . Sio tu kwamba ninathamini sana fursa hii, lakini pia nataka kuifanikisha. Mabadilishano ya tamaduni huambatanisha ulimwengu zaidi. |
|
UZOEFU WA KITAALUMA
SIFA
|